Sunday, August 10, 2014

Mwanzo wa kuvuma: Na Vitali Maembe.

Vuma!


Katikati ya mwezi Julai 2014 niliwasiliana na Vitali na akaniambia baada ya siku mbili atakuja studio, anazo nyimbo anataka kurekodi. Mimi nilimeza maneno yake kupitia masikio yangu, nikaendelea na shughuli za kawaida.
Baada ya siku mbili Maembe alinipigia simu kunieleza kuwa yupo njiani anakuja studio. Hadi muda huo nilikuwa sijajitayarisha kwa ujio wake. Haikuwa tatizo. Wakati natafakari nini kitafanyika, Nelly akanipigia simu kunieleza kuwa anakuja studio. Ilikuwa afadhali sana maana wiki hiyo nilimtegemea Nuru atakuwapo studio kwa kadhaa zilizokuwapo kipindi hicho. Na mimi niliwasiliana na 'Mugabe' (aka Sindimba Tete) tuweze kupata uwepo wake pia.
Kwenye muda wa saa tano, Maembe alifika na vijana wake wawili - Hussein na mwingine yule anapiga ngoma. Nakumbuka hatua za mwanzo za 'kuvumisha' zilianza kwa ushiriki wangu kidogo baada ya hapo Nelly aliendelea.