Thursday, June 12, 2014

Muziki wa Reggae unakufa?


Kwa miaka takriban kumi, muziki wa Reggae umesambaa kwa kasi katika kona nne za dunia. Teknolojia imechangia sana katika mabadiliko yaliyotokea - kuanzia kwenye uandishi, midundo na utamaduni unaoambatana na muziki huo.

Yupo mwandishi mmoja anaitwa Davina Hamilton wa huko Uingereza, amewahi kuuliza kama 'Muziki wa Reggae Umekufa?'. Katika makala yake, alihojiana na wadau tofauti; ambao walifafanua kutokana na mazingira yao. Mwandishi huyo wa habari za burudani, alirudia tena kuandika 'Kifo cha polepole' na kumalizia kwa kuandika kuwa muziki wa Reggae umetawala sana na kuzoeleka katika mfumo uliopo, ndio maana hakuna mtu anayegundua kuwa bado unaishi. Kwa maana, umekuwa wa kawaida sana.


Takwimu za mauzo katika nchi za Marekani na zile za Ulaya zinaonyesha kushuka sana kwa mauzo ya santuri za Reggae. Utafiti kuhusu uhudhuriaji wa wapenzi wa muziki huo, unatofautiana kwa sehemu mbali mbali. Pamoja na mijadala ambayo imetokea, maswali bado yanaulizwa. Angus Taylor (mwandishi) anataka kujua kuhusu kushuka kwa mauzo - 'Inamaanisha nini?.






No comments:

Post a Comment