Ureno v Ujerumani (Group G)
Ujerumani na Ureno ni mataifa mawili ambayo yapo katika nafasi tano za juu katika viwango vya FIFA, na wote wana uwezo wa kufanya maajabu katika Kombe la Dunia 2014.
Ureno ni timu ngumu kuitabiri. Walihitaji mchujo kupata ushindi dhidi ya Sweden kufikia fainali za Kombe la Dunia. Walipoteza mchezo mmoja tu katika kufuzu, lakini walifungwa na Israel mara mbili.
Suala kubwa kwa Ureno wiki chache zilizopita limekuwa afya ya nyota wao Christiano Ronaldo. Amekuwa akikabiliana na tatizo kwenye mguu. Ronaldo ana uwezo wa kubeba mafanikio yao, ila tatizo lao kidogo limekuwa ni ukosefu wa mshambuliaji wa kati, lakini pembeni wamekamilika.
Kwa upande mwingine, Ujerumani wamejikuta wanashughulika na majeruhi mengi. Marco Reus atakosa mashindano kutokana na kuumia kifundo cha mguu. Kipa Manuel Neuer ni mmoja wa makipa bora dunia, lakini alikuwa uliumia bega. Yeye atacheza. Kiungo Bastian Schweinsteiger aliumia goti mwezi uliopita, lakini yeye pia anatarajiwa kuwa fit.
Ujerumani ni moja ya taifa linalotarajiwa kushinda mashindano haya. Walikuwa moja ya timu zilizofanya vizuri zaidi katika kufuzu, kwa kushinda michezo tisa na kutoka sare moja, na kufunga mabao 36 katika mechi 10.
Hizi ni timu mbili bora katika dunia, na Ujerumani kati ya timu zinazitarajiwa kunyakua Kombe la Dunia 2014; bila kusahau kuwa Ureno ina mchezaji bora duniani - Ronaldo.
Ngamia ametabiri mshindi!!

No comments:
Post a Comment