Edinson Cavani yupo tayari kubeba mzigo kutokana na kukosekana kwa Luis Suarez kwa Uruguay kwenye mechi ya kwanza ya Kombe la Dunia 2014. Suarez alikuwa kwenye matibabu ya goti lake la kushoto.
Uruguay walimaliza nafasi ya nne miaka minne iliyopita kule Afrika Kusini, mchango mkubwa ulitokana na magoli matano ya Diego Forlan, ambayo yalimwezesha kupata heshima ya mpira wa dhahabu. Sasa Uruguay itakutana na Costa Rica katika mechi yao ya kwanza.
Costa Rica itawatuma mashujaa wao wa mabao, pamoja na kiungo Bryan Ruiz, ambaye amepachika mabao 12 katika mechi 63 tangu mwaka 2005. Atakayekuwapo pamoja na Ruiz ni Joel Campbell mwenye umri wa miaka 21 - ambaye wakati wa mzunguko wa kufuzu, Campbell pia alipachika bao moja katika mechi tano.



No comments:
Post a Comment