Friday, June 13, 2014
Kombe La Dunia 2014 - GHANA
Asamoah Gyan alifunga goli dhidi ya Korea Kusini na katika kushangilia, wachezaji wa timu ya taifa ya Ghana wakajikita katika Azonto, ngoma maarufu kutoka Ghana.
Ushindi dhidi ya timu ya Marekani miaka minne iliyopita uliipeleka timu ya taifa ya Ghana katika robo fainali za Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza. Ghana ulikubalika kama "Timu ya Afrika" - ilitegemewa kuwa nchi ya kwanza kutoka Afrika kufikia nusu fainali, lakini kupoteza mechi kwa Urugwai kwa mikwaju ya penati; safari ilikomea hapo.
Waghana wanayo kila sababu ya kuwa na matumaini, kwa sababu ya kuweza kuwaondoa Marekani katika mashindano mawili mfululizo ya Kombe la Dunia. Basi itabidi tujitayarishe kwa Azonto nyingine.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



No comments:
Post a Comment