Wednesday, September 24, 2014

Irie Productions.

Irie Productions


Mwaka 2009, nilianza kutengeneza studio za Irie Productions, huku kwetu Tegeta. Hii ilikuwa miaka miwili baada ya projects tulizofanya tulipokuwa na akina Tony pale ActiveAudio - Manzese. Mwaka 2011 ndio nilifungua milango kwa jamii kuweza kurekodi kazi zao, wakati huo hakuna ala - zaidi ya Akai MPK61 na iMac. Tulitoa nafasi kwa wasanii wa hapa jirani na mazingira yetu; na jaribio hilo halikuwa na matunda. Maana wengi walihitaji hatua zaidi ya kurekodi tu. Walihitahi label na promosheni za redio.
Marafiki, ndugu na jamii ya wasanii; na kwa kiasi fulani wale waliopo kwenye fani ya habari. Walikuwa wananishauri na kuniambia kuwa nina msimamo usioeleweka - kwa nini nisifanye kwa kiwango kikubwa. (Nikafikiria - 'ukubwa wa pua sio wingi wa kamasi'). Wewe Gotta unafahamika, unaweza kufanya vitu kadhaa, unajuana na watu wengi. (Nikafikiria - 'sitaki wanijue mimi, lakini nataka wajue nini kitatoka Irie Productions').