Wednesday, December 2, 2015

Biashara ya muziki: Kabla na Baada.

Biashara ya muziki.


Mwaka 2004 niliandika kitabu kuhusu biashara ya muziki. Kwa wakati huo kitabu hicho “Introduction To Music Business” kilishabihiana na mazingira ya wakati huo.
Miaka michache iliyopita, dunia ilitegemea mabadiliko makubwa kwenye biashara ya muziki kutokana na kuingia kwenye mfumo wa dijitali (digital). Upatikanaji wa bidhaa za muziki kupitia mtandao wa intaneti, ilikuwa furaha kwa mtumiaji. Na urahisi wa kupata wimbo mmoja badala ya kununua toleo lote la albamu fulani, na kwa gharama nafuu.

Katika suala la uchumi kwenye biashara ya muziki ni kipigo kwa msanii. Labda kwa wasanii wakubwa na wenye uwezo wa kulazimisha mkataba wenye makato ya juu.
Kwa uhalisia, kampuni ya uaandaji wa muziki ‘lebo’ – ni mwekezaji. Unapokuwapo mkataba; lebo inabeba gharama za kurekodi, kusambaza na kuitambulisha pia. Lebo inafanya hivyo kwa makubaliano ya makato kutoka kwenye mauzo.  Na huo ndio mfumo ulivyo, hadi tulipofikia mfumo wa kidijitali.