Irie Productions
Mwaka 2009, nilianza kutengeneza studio za Irie Productions, huku kwetu Tegeta. Hii ilikuwa miaka miwili baada ya projects tulizofanya tulipokuwa na akina Tony pale ActiveAudio - Manzese. Mwaka 2011 ndio nilifungua milango kwa jamii kuweza kurekodi kazi zao, wakati huo hakuna ala - zaidi ya Akai MPK61 na iMac. Tulitoa nafasi kwa wasanii wa hapa jirani na mazingira yetu; na jaribio hilo halikuwa na matunda. Maana wengi walihitaji hatua zaidi ya kurekodi tu. Walihitahi label na promosheni za redio.
Marafiki, ndugu na jamii ya wasanii; na kwa kiasi fulani wale waliopo kwenye fani ya habari. Walikuwa wananishauri na kuniambia kuwa nina msimamo usioeleweka - kwa nini nisifanye kwa kiwango kikubwa. (Nikafikiria - 'ukubwa wa pua sio wingi wa kamasi'). Wewe Gotta unafahamika, unaweza kufanya vitu kadhaa, unajuana na watu wengi. (Nikafikiria - 'sitaki wanijue mimi, lakini nataka wajue nini kitatoka Irie Productions').

























